{"id":159,"date":"2017-02-17T12:54:26","date_gmt":"2017-02-17T09:54:26","guid":{"rendered":"http:\/\/endtimecog.org\/html\/?p=159"},"modified":"2017-02-17T12:54:26","modified_gmt":"2017-02-17T09:54:26","slug":"huyu-ni-shetani","status":"publish","type":"post","link":"https:\/\/endtimecog.org\/html\/huyu-ni-shetani\/","title":{"rendered":"HUYU NI SHETANI!"},"content":{"rendered":"<p><span class=\"fontstyle2\">Tunaishi katika ulimwengu ambao ni wachache sana wanaoufahamu. Muulize mtu ye yote yule kuhusu cho chote kile kihusucho maisha, majibu utakayopata yatakuwa ni ya kubahatisha tu; hayana uthabiti wo wote. Mashirika yetu ya uma yana tamaduni na mila zinazotumika kuongoza watu katika namna ya kuishi na kuhusiana wao kwa wao. Ukiziangalia hizi tamaduni na mila, utakuta kwamba zinafuatiliwa kulingana na matakwa ya walio wengi.<\/span><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle2\"><br \/>\nKwa hivyo, kila mtu hufanya na kuishi kwa kuwatazama wengine kama kioo chake; yaani, mtu hutenda kwa kuzingatia jinsi wengine wasemavyo, wanavyoonelea, na ni kipi kitawapendeza, n.k. Naam, ni mfumo ambao mtazamo wake ni wa kibinadamu. Matokeo ya kuishi hivyo, kujaribu kuishi kulingana na maoni, matakwa na mapenzi ya wengi, kumeleta vurugu na ukosefu wa haki. Katika jitihada za<br \/>\nkutafuta kibali mbele ya wanadamu wenzetu, tumeishi maisha yenye huzuni na mifadhaiko.<\/span><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle2\"><br \/>\nMtu anaweza kuogopa kutenda haki kwa sababu walio wengi hawakubaliani nayo. Anapokataliwa na walio wengi, anaona haya na kujiona duni kwa wengine. Anapokubalika, anafurahia na kujiona kuwa shujaa, na hujigamba huku akiendelea kutafuta kupendwa zaidi na watu. Lakini tukiangalia matokeo ya kupendwa ama kutopendwa, tunaona yakiwa sawa. Anayepuuzwa <\/span><span class=\"fontstyle3\">{asiyependwa} <\/span><span class=\"fontstyle2\">hupigana<br \/>\nkutafuta kukubalika na kuonesha msimamo wake mbele ya wengine. Anayekubalika <\/span><span class=\"fontstyle3\">{anayependwa} <\/span><span class=\"fontstyle2\">naye pia hupigana kujaribu kuwafanya wengine wapuuzwe ili abaki kuwa mwenye kusifiwa peke yake. Ukweli ni kwamba, huu mfumo umeleta vurugu na vita katika ulimwengu wa leo. Pia umewafanya wanadamu kuwa watumwa wa wenzao, na wakifikiria mambo ya wanadamu tu; yaani, <\/span><span class=\"fontstyle0\">&#8220;wananionaje,<br \/>\nwananisemaje, wanapendezwaje, n.k.\u201d<\/span><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle2\">Jambo hili limewafanya karibu watu wote kuishi maisha ya kuabudiana wao kwa wao, huku wakijibidiisha kufikia kile kiwango kilichowekwa na wenzao. Watu hung\u2019ang\u2019ania kupendwa, kukubalika na kuungwa mkono. Pia hujitahidi kujiepusha mbali na yale yawezayo kuwafanya wapuuzwe, hata kama ndiyo mazuri na ya haki.<\/span><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle2\"><br \/>\n<\/span><span class=\"fontstyle0\">MATOKEO YAKE<\/span><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle0\"><br \/>\n<\/span><span class=\"fontstyle2\">Baada ya watu kujipangia na kudumu katika huo mfumo ambao ndio huitwao <\/span><span class=\"fontstyle0\">&#8220;ulimwengu wa leo\u201d, <\/span><span class=\"fontstyle2\">wanadamu wamefikia katika hali gani ya maisha? Amini usiamini, lakini ukweli ni kwamba; matokeo ya kuufuata huo mfumo wa wanadamu kuangaliana na kuabudiana wenyewe, ni hizi shida tunazoziona hivi sasa. Katika hizo jitihada za mtu kujiweka panapokubalika na wenzake, kumetokea<br \/>\nmalumbano yasio na mwisho. Jamii zinazidi kuvunjika, serikali zinaendelea kupinduliwa, uongo umeongezeka huku kila mtu akijaribu kumnyang\u2019anya mwenzake kwa namna moja ama nyingine; wizi wa mabavu, vita ambavyo vimewafanya watu kufa maji wakikimbilia kwenye usalama, vifo vitokanavyo na mangonjwa yasiyo na tiba, uchafuzi wa mazingira ambao umeleta mabadiliko ya hali ya hewa<br \/>\nyanayosababisha mafuriko, vimbunga vikali, na mengine mengi. Haya yote yanathibitisha wazi kwamba, huu mfumo, mila na tamaduni zake, una kasoro kubwa sana!<\/span><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle2\"><br \/>\nNi kasoro gani hiyo? Tulianza kwa kusema kwamba, ulimwengu wa leo haujitambui; na sasa huo usemi unathibitishwa na haya matokeo mabaya ya maisha yasiyo na ufahamu. Haya matokeo yanazidi kuwa mabaya kila uchao mpaka watu wameanza kuyaona maisha kama yasiyo na maana kamili. Karibu kila mtu anaishi kwa woga na kutojua kitakachojiri baada ya kuona jinsi wengi wanavyoangamia na<br \/>\nwengine kupatwa na madhara mbali mbali kwa ghafla. Watu sasa wamebaki kushangaa na kujiuliza kama kweli kuna Mungu ambaye anayaona haya yote huku akikaa kimya bila kufanya cho chote ili kuokoa <\/span><span class=\"fontstyle2\">katika hali hii. Na ili tupate jibu sahihi, inatubidi tutafute chanzo cha huu mfumo na mwanzilishi wake.<\/span><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle2\"><br \/>\nTutatafuta wapi basi? <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Yuko Mungu mbinguni afunuaye siri&#8221; (Danieli 2:28), <\/span><span class=\"fontstyle2\">atatujulisha aliyeanzisha huu mfumo ambao umeleta maovu haya yote<\/span><span class=\"fontstyle0\">. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Baada ya kumwuumba mwanadamu, Mungu alimwagiza kuhusu namna apaswavyo kuishi. Na hayo maagizo yahusuyo maisha ndiyo kile kupitia kwa manabii na mitume kiliandikwa kikawa ile biblia uisomayo leo. Kuhusu haya maagizo, muumba wetu anatuambia, <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Wana amani nyingi waipendao sheria yako, Wala hawana la kuwakwaza&#8221; Zaburi 119:165. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Je! hili si kinyume cha yale maisha tuyaonayo leo ya vita na vikwazo tele, kuthibitisha kwamba haya ndiyo maisha ya kweli? Anazidi kuthibitisha hayo akisema, <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Maana ni uhai kwa wale wazipatao, Na afya ya mwili wao wote&#8221; Mithali 4:22.<\/span><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle4\"><br \/>\n<\/span><span class=\"fontstyle2\">Sasa basi, kwa mujibu wa haya maagizo ya Mungu muumba ambayo ndiyo maelezo sahihi kuhusu maisha; je! Mungu anasema kwamba mwanzilishi wa haya maisha maovu ya kutatanisha ni nani? Hebu tufuatilie tafadhali. Baada ya kumwambia Adamu haya maagizo ya maisha mazuri, Mungu pia alimuonya kuhusu maisha ambayo ni ya uharibifu, na ambayo yatamuua endapo akiyafuata. Sikiliza vile alivyomwambia, na ambavyo ndivyo pia akuambiavyo wewe leo usomaye ujumbe huu ikiwa unatafuta kuishi vizuri kwa Amani na furaha. Anasema: <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika&#8221; Mwanzo 2:17. <\/span><span class=\"fontstyle3\">(kwa maelezo zaidi kuhusu huu mti, agiza ujumbe wetu usemao, <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;MITI MIWILI\u201d, <\/span><span class=\"fontstyle3\">ili ujifunze zaidi, utatumiwa bure). <\/span><span class=\"fontstyle2\">Ukisoma <\/span><span class=\"fontstyle4\">Mwanzo 3:4-6, <\/span><span class=\"fontstyle2\">utaona kwamba mwanadamu alishawishiwa na Shetani, na akafanya kinyume na maagizo ya Mungu, akala yale matunda aliyokatazwa kula. Kwa hivyo sasa, tumepata jibu la swali letu; kwamba, aliyeanzisha haya maisha mabaya ya uharibifu si Mungu, bali ni Shetani. Alimwambia mwanadamu kwamba, Mungu aliye muumba wake amemdanganya. Lakini je! Shetani yeye alisema ukweli?<br \/>\nMungu ambaye kama vile tulivyoona mwanzoni, ndiye peke yake ajuaye na afunuaye siri, anatuambia kuwa Shetani ni mwongo, maana anasema, <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;yeye <\/span><span class=\"fontstyle3\">(Shetani) <\/span><span class=\"fontstyle4\">ni mwongo, na baba wa huo&#8221; Yohana 8:44. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Tena,<\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;\u2026aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote&#8230;&#8221; Ufunuo 12:9.<\/span><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle4\"><br \/>\n<\/span><span class=\"fontstyle2\">Haya yanazidi kuthibitisha kile tulichoanzia kusema kwamba, karibu watu wote leo hawajui cho chote kuhusu maisha. Na hii ni kwa sababu kile walichopokea na kukubaliana nacho kama mwongozo <\/span><span class=\"fontstyle3\">(ufahamu) <\/span><span class=\"fontstyle2\">wa maisha kutoka kwa Shetani ni uongo. Mungu akiyathibitisha haya anatuambia: <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Hakuna afahamuye; Hakuna amtafutaye Mungu. Wote wamepotoka, wameoza wote pia: Hakuna mtenda mema, la! hata mmoja&#8230; Wala njia ya amani hawakuijua&#8221; Warumi 3:11-12, 17. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Kutokana na huu ujinga, watu wanamlaumu Mungu kwa haya mabaya yote yanayoendelea. Wameendelea kulaumu hata kufikia kiwango cha kumwona Mungu kama mwenye upendeleo. Kama anayependelea kabila zingine zaidi ya zingine. Basi elewa sasa kwamba, si Mungu aliyeuleta huu uovu, bali ni Shetani, na ndiye<br \/>\nmwenye kuwafanya watu waoneshe huu upendeleo. <\/span><span class=\"fontstyle3\">(kwa maelezo ya kina zaidi, agiza ujumbe wetu usemao, &#8220;<\/span><span class=\"fontstyle4\">SHETANI NI NANI?\u201d, <\/span><span class=\"fontstyle3\">ili ujifunze zaidi).<\/span><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle2\">Sasa basi, tumejua chanzo cha ubaya na uovu wote uliyomo ulimwenguni leo. Tufanye nini sasa ili tujiepushe nao na tuweze kuishi maisha ya ushirikiano yenye Amani na furaha?<\/span><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle2\"><br \/>\n<\/span><span class=\"fontstyle0\"><strong>TUBUNI<\/strong><br \/>\n<\/span><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle2\">Ukishajua kikulacho, kama mtu mwenye busara, utafanya nini? Utaendelea kushikamana nacho? Sio rahisi. Kile utakachofanya haraka iwezekanavyo ni kuachana na kitu hicho na kujitenga mbali nacho kabisa. Na hivyo ndivyo Mungu katika Kristo yesu anavyotuagiza akisema, &#8220;<\/span><span class=\"fontstyle0\">tubuni\u201d. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Neno <\/span><span class=\"fontstyle0\">&#8220;kutubu&#8221; <\/span><span class=\"fontstyle2\">lina maana ya, &#8220;<\/span><span class=\"fontstyle0\">kugeuka&#8221;, <\/span><span class=\"fontstyle2\">ama <\/span><span class=\"fontstyle0\">&#8220;kuacha\u201d. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Kwa hivyo basi, suluhisho ni kuacha kuishi kwa kuufuata<\/span><br \/>\n<span class=\"fontstyle2\">huu uongo wa Shetani, na tuanze kuishi kulingana na kile Mungu atuambiacho katika Maandiko. Na ili tufaulu kufanya hivyo, inabidi kwanza tuache kutumia akili zetu kujaribu kupanga mambo vile tunavyoonelea wenyewe, maana Mungu anawaambia wale waliotubu <\/span><span class=\"fontstyle3\">(waliogeuka kuachana na udanganyifu wa Shetani) <\/span><span class=\"fontstyle2\">kwamba, <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Mtumaini BWANA kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili<br \/>\nzako mwenyewe; Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako&#8221; Mithali 3:5-6. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Hivyo basi, inatubidi kuanza upya kama watoto wachanga waliozaliwa hivi sasa. Lazima turudi kwa Mungu ili atuambie sisi ni nini, tunafanya nini hapa, na ni nini hatima <\/span><span class=\"fontstyle3\">(mwisho) <\/span><span class=\"fontstyle2\">ya maisha yetu? Majibu ya haya maswali ndiyo yaliyoandikwa na yakaitwa Biblia, yaani, Maandiko Matakatifu. <\/span><span class=\"fontstyle3\">(soma ujumbe<br \/>\nwetu usemao, &#8220;<\/span><span class=\"fontstyle4\">MWANADAMU NI NANI?&#8221;, <\/span><span class=\"fontstyle3\">kwa maelezo ya kina zaidi).<\/span><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle3\"><br \/>\n<\/span><span class=\"fontstyle2\">Kwa hivyo basi, muumba wetu anasema sisi ni nini? Naam; anasema, <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;BWANA Mungu akamfanya Mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai&#8221; Mwanzo 2:7. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Kwa hivyo basi; Wewe ni mavumbi. Nani kasema? Je! ni sisi? Sio sisi tusemao hayo, bali ni yeye aliyekuumba, na ambaye peke yake ndiye akufahamuye. Ikiwa tutatubu <\/span><span class=\"fontstyle3\">(tutageuka), <\/span><span class=\"fontstyle2\">ni lazima tuanze kwa kukubali kwamba sisi ni mavumbi. Kwa mujibu wa uongo wa Shetani; ni kwamba wewe ni kama Mungu na wala wewe sio mavumbi; tena kwamba Wewe huwezi kufa, una roho isiyokufa ndani yako <\/span><span class=\"fontstyle4\">(soma Mwanzo 3:4-5). <\/span><span class=\"fontstyle2\">Hapa ndipo siri kubwa ya uongo wa Shetani ilipofichwa, na ndio chanzo cha uovu na uharibifu wote tunaoushuhudia ulimwenguni leo. Tunasema hivyo kwa nini? Maana baada ya kuukubali uongo kwamba sisi ni kama Mungu; basi kilichofuata ni sisi kujidhania na kujitumainisha kuwa tu wakamilifu na tusioweza kukosea, yaani tunaojua kila kitu. Kwa sababu hiyo, jirani yako anapokukosea; basi unasema kwamba anafanya makusudi, ni ujeuri tu. Tena<br \/>\nanapowezeshwa na Mungu kutenda wema; basi unasema ni mwenye hekima, anafaa kuabudiwa na kupewa sifa. Katika huu mfumo wa uongo, Shetani anahakikisha kwamba, hakuna kusameheana kabisa, bali ni kulipiza kisasi tu; na kwa njia hii, amewasha moto usiozimika duniani. Hii ndiyo sababu unaona umoja wa mataifa waking&#8217;ang&#8217;ana kuleta Amani; na badala yake,vita vinazidi kusambaa kila kona<br \/>\nduniani.<\/span><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle2\"><br \/>\nLakini Mungu ambaye peke yake ndiye mkweli anasema kinyume na Shetani. Anatukumbusha kwamba hatujui cho chote, maana anatuambia kwamba; <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Mtu asijidanganye mwenyewe; kama mtu akijiona kuwa mwenye hekima miongoni mwenu katika dunia hii, na awe mpumbavu <\/span><span class=\"fontstyle3\">(yaani, atubu), <\/span><span class=\"fontstyle4\">ili apate kuwa mwenye hekima <\/span><span class=\"fontstyle3\">(kwa kuishi kwa maelekezo ya Mungu). <\/span><span class=\"fontstyle4\">Maana hekima ya dunia hii ni<br \/>\nupuzi <\/span><span class=\"fontstyle3\">(ni uongo na ujinga) <\/span><span class=\"fontstyle4\">mbele za Mungu&#8230; &#8221; 1 Wakorintho 3:18-19. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Ufahamu wa kweli wa kuhusiana na mwanadamu mwenzako anapotenda wema au ubaya ulioneshwa na bwana wetu Yesu Kristo ambaye ndiye Mjumbe tuliyetumiwa na Mungu kuja kutufundisha maisha halisi. Wakati watu walipomtendea mabaya, hata wakati walipokuwa wakimuua, yeye hakupigana kulipiza kisasi. Na badala<br \/>\nyake; alisema, <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo&#8221; Luka 23:34. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Je! alikuwa akisema hivyo kwa kujifanya tu? La, hasha. Bali alimwamini Mungu kwamba, wanadamu wamedanganyika na hivyo wanauita wema kuwa ni ubaya, na ubaya kuwa ni wema.<br \/>\nStefano ambaye alimwamini Yesu, aliyarudia maneno hayo hayo wakati alipokuwa akipigwa kwa mawe akisema; <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Bwana, usiwahesabie dhambi hii&#8221; Matendo 7:60. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Je! wote hawa walikua wakiongea hivyo kwa unafiki na kujifanya tu? Je! walikuwa wakiyanena hayo huku wakiwa na hasira na chuki nyingi dhidi ya hao watesi wao? Sivyo hata kidogo. Bali ni watu walioamini na kuyakubali yale Mungu<br \/>\nasemayo kwamba, <\/span><span class=\"fontstyle0\">&#8220;hakuna aliye na ufahamu, wala aliye mwema, maana bado hatujakamilishwa tukawa kama Mungu ambaye peke yake ndiye mwema na mwenye ufahamu wa kweli&#8221;, <\/span><span class=\"fontstyle4\">soma Matendo 19:17.<\/span><br \/>\n<span class=\"fontstyle2\">Pia, kwa habari ya kupokea sifa kutoka kwa wanadamu wasiofahamu kwamba ni Mungu ndiye amwezeshaye mtu kutenda wema; Yesu ambaye ndiye anayetufundisha maisha ya Mungu ya kweli, hakukubali sifa zimwendee yeye badala ya Mungu. Wanadamu walipomjia wakimwita mwema; aliwaambia, <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Hakuna aliye mwema ila Mungu peke yake&#8221;, soma Mathayo 19:17. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Alimaanisha nini? Alimaanisha kwamba, kama kuna mtu atendaye wema, basi huo wema amepewa na Mungu. Mtu huyo ni kama gitaa lichezwalo, na hivyo, sifa zinafaa zimwendee mcheza <\/span><span class=\"fontstyle3\">(au mpiga) <\/span><span class=\"fontstyle2\">gitaa na sio gitaa lenyewe.<\/span><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle2\"><br \/>\nHili linathibitika kwa Paulo, alipotenda maajabu <\/span><span class=\"fontstyle3\">(miujiza) <\/span><span class=\"fontstyle2\">huko Efeso na watu wakataka kumwabudu <\/span><span class=\"fontstyle3\">(kumsifu). <\/span><span class=\"fontstyle2\">Yeye alikataa akawaambia, <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Akina bwana, mbona mnafanya haya? Sisi nasi tu wanadamuhali moja na ninyi; twawahubiri habari njema, ili mgeuke <\/span><span class=\"fontstyle3\">(mtubu) <\/span><span class=\"fontstyle4\">na kuyaacha mambo haya yaubatili na kumwelekea Mungu aliye hai, aliyeumba mbingu na nchi na bahari na vitu vyote vilivyomo&#8221; Matendo 14:15. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Na hata malaika wenyewe wanajua ya kwamba, ni Mungu peke yake ndiye anayefaa kusifiwa kwa kila jambo jema wanalofanya wanadamu. Yohana alipotaka kumwabudu malaika, aliambiwa, <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Angalia, usifanye hivi; mimi ni mjoli wako na wa ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu. Msujudie Mungu&#8221; Ufunuo 19:10. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Je! hao nao walikuwa wanajua wayasemayo ama hawakujua?<br \/>\nTangu lini watu wakakataa sifa? Watu hawa <\/span><span class=\"fontstyle3\">{akina Stefano, Paulo n.k.} <\/span><span class=\"fontstyle2\">walijua kwamba wao ni udongo <\/span><span class=\"fontstyle3\">(mavumbi) <\/span><span class=\"fontstyle2\">ambao bado uko katika mikono ya mfinyanzi. Kwa hivyo basi, cho chote kile kilicho chema kinachotendeka maishani mwao, ni mfinyanzi <\/span><span class=\"fontstyle3\">(muumbaji) <\/span><span class=\"fontstyle2\">ndiye atendaye na wala sio wao. Walijua vizuri sana kwamba, sisi wanadamu wa kimwili sasa hivi hatuna uwezo wa kutengeneza ufahamu. Akili zetu hutegemea kujifunza kutoka kwa Mungu au kwa Shetani. Naam, ukweli ni kwamba; ufahamu wetu hutokana na mafundisho yatokayo katika ulimwengu wa roho, ambapo kila mwanadamu anajiunga kufundishwa ama na Mungu au na Shetani; na hivyo, anakuwa mtumwa wa yule amfundishaye. Wema ni wa Mungu, na ubaya ni wa Shetani. Na hii ndiyo maana, badala ya kumlaumu anayemtumikia Shetani<br \/>\natendapo ubaya; wanamhurumia mtu huyo, maana wanajua kuwa yeye ni mtumwa. Maana imeandikwa: <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Hamjui ya kuwa kwake yeye ambaye mnajitoa nafsi zenu kuwa watumwa wake katika kumtii, mmekuwa watumwa wake yule mnayemtii, kwamba ni utumishi wa dhambi uletao mauti, au kwamba ni utumishi wa utii uletao haki&#8221; Warumi.6:16. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Hii ndio sababu pia, mtu alipotenda mema, walijua<br \/>\nkwamba ni Mungu ndiye atendaye ndani ya mtu huyo, na hivyo walimsifu Mungu; yaani, walikataa <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;kuabudu kiumbe badala ya kumwabudu yeye aliyekiumba&#8221;, soma Warumi 1:24. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Unaona sasa jinsi ambavyo ulimwengu umechanganyikiwa, na kwamba badala ya kufuata maagizo ya Mungu ili waishi vizuri kwa Amani; wanafuata uongo wa Shetani huku wakitumia fikira na mawazo yao wenyewe? <\/span><span class=\"fontstyle3\">(kwa maelezo zaidi, agiza ujumbe wetu usemao, &#8220;<\/span><span class=\"fontstyle4\">UJUZI WA MAWASILIANO&#8221;, <\/span><span class=\"fontstyle3\">ili ujifunze zaidi, utatumiwa bure ujumbe huo).<br \/>\n<\/span><span class=\"fontstyle2\">Wapendwa wetu; huku kutojijua, pamoja na watu kuukubali uongo wa Shetani na kuutumia kama ufahamu wa maisha, ndiko kumeleta hizi vurugu zote tunazoziona duniani leo. Wakijidhania kujua na kujichukulia kuwa kama miungu, basi kila mmoja anang\u2019ang\u2019ana na kupigana na mwenzake, aitha akitaka kusifiwa, ama akipinga kudharauliwa. Ni kweli kwamba, Mungu alituahidi kutufanya kuwa<br \/>\nmiungu; lakini kwa sasa, sisi ni mavumbi. Ni mpaka pale ambapo tutakamilishwa; lakini kwa sasa hivi hatuna cha kusifiwa wala kulaumiwa, maana kwa sasa sisi ni watumishi wa wema wa Mungu au wa ubaya wa Shetani. Hii ndiyo sababu Mungu anatuambia kwamba, <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama <\/span><span class=\"fontstyle3\">(yaani, si dhidi ya wanadamu); <\/span><span class=\"fontstyle4\">bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho&#8221; Waefeso 6:12.<\/span><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle4\"><br \/>\n<\/span><span class=\"fontstyle2\">Tufanye nini basi? Tutubuni <\/span><span class=\"fontstyle3\">(tugeukeni), <\/span><span class=\"fontstyle2\">tuache kuutumia uongo wa Shetani, na badala yake, tuanze kuutumia ukweli wa Mungu kama ufahamu wa maisha mema na makamilifu. Tuache kabisa kujidanganya kuwa tunajua; na badala yake, tuanze upya kabisa, maana Mungu anatushauri kwamba, <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Mtu asijidanganye mwenyewe; kama mtu akijiona kuwa mwenye hekima miongoni mwenu katika dunia hii, na awe mpumbavu <\/span><span class=\"fontstyle3\">(yaani, akubali kwamba hujui cho chote), <\/span><span class=\"fontstyle4\">ili apate kuwa mwenye hekima<\/span> <span class=\"fontstyle3\">(kwa kujifunza kwa Mungu)&#8221; <\/span><span class=\"fontstyle4\">1 Wakorintho 3:18. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Naam; tukubali kwamba kile tulichokitumia miaka yote hii kama ufahamu wa maisha ni uongo. Kwa hivyo sasa, ni juu yako wewe unayeusoma ujumbe huu kufanya uamuzi. Je! utaendelea kuishi kwa kuufuata uongo wa Shetani uliokudanganya kwamba wewe ni<br \/>\nkama Mungu, ama utaukataa tangu sasa na uanze kujifunza kwa Mungu ukweli ambao Mungu atautumia kukuumba akili na mawazo yako ili yawe kama yale yake, na mwishowe akufanye kuwa kiumbe wa kiroho kama yeye? Kama unataka kujifunza ukweli; basi Mungu anakuambia uanze kwa kufahamu kwamba, <\/span><span class=\"fontstyle0\">&#8220;wewe ni mavumbi <\/span><span class=\"fontstyle3\">(udongo), <\/span><span class=\"fontstyle0\">na wala sio Mungu&#8221;, <\/span><span class=\"fontstyle4\">soma Mwanzo 3:19. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Na tena ufahamu<br \/>\nkwamba, <\/span><span class=\"fontstyle0\">&#8220;wewe ni kama nyasi, na maisha yako ni kama maua ambayo hunyauka baada ya muda mfupi tu&#8221;, <\/span><span class=\"fontstyle4\">soma Isaya 40:6-7. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Na zaidi ya hayo, ujue ya kuwa, <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke Siku zake za kuishi si nyingi, naye hujaa taabu&#8221;, soma Ayubu 14:1-2. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Ikiwa utakubaliana na hayo; basi sasa wewe uko tayari kuanza upya kijifunza kwa Mungu. Naye Mungu anasema tufanye nini baada ya kuyakubali hayo?<\/span><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle2\"><br \/>\n<\/span><strong><span class=\"fontstyle0\">THAMANI YA MAVUMBI<\/span><\/strong><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle0\"><br \/>\n<\/span><span class=\"fontstyle2\">Wale wote waliotangulia mbele yetu ambao walimwamini Mungu na kuanza kujifunza kwake, katika maandiko wanashuhudia ukweli huu. Ibrahimu ambaye Yesu Kristo alizaliwa kutokana na uzao wake, alitambua na kukiri akisema, <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;&#8230; nami ni mavumbi na majivu tu&#8221; Mwanzo 18:27. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Daudi ambaye alishuhudiwa kuwa na roho kama ile ya Mungu anasema, <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Kwa maana Yeye <\/span><span class=\"fontstyle3\">(Mungu)<\/span><span class=\"fontstyle4\">anatujua umbo letu, Na kukumbuka ya kuwa sisi tu mavumbi&#8221; Zaburi 103:14. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Nabii Isaya anathibitisha huu ukweli wa Mungu akisema, <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;&#8230; sisi tu udongo\u2026 sisi sote twanyauka kama jani\u201d Isaya 64:8,6. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Paulo naye anaongezea kasema, <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Kwa maana najua ya kuwa ndani yangu, yaani, ndani ya mwili wangu, halikai neno jema&#8221;Warumi7:18.<br \/>\n<\/span><span class=\"fontstyle2\">Baada ya kuupata huu ukweli wote kutuhusu sisi wanadamu; sasa basi, hebu tuone ile siri ya udanganyifu wa Shetani inavyofanya kazi; na ambayo ndiyo sababu Mungu anawaagiza wote watakao kutoka katika huo uongo wajikane kwanza nafsi zao na kuachana kabisa na\u00a0 mwenendo wa awali.<\/span><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle2\"><br \/>\nNi kitu gani katika mavumbi ambacho ni cha thamani kiasi kwamba utakitetea na kukishikilia? Mavumbi yako kila mahali. Tunayakanyanga, tunayatupia takataka, vinyesi n.k. Siku moja, nilitembelewa na marafiki zangu nyumbani kwangu. Na walipokuwa wakitembea hapa na pale; hili wazo la mavumbi likanijia akilini. Niliwaangalia wakiyakanyanga mavumbi na wala hakuna aliyekuwa na haja nayo.<br \/>\nNikajiuliza; \u201c<\/span><span class=\"fontstyle0\">kama haya mavumbi yangekuwa ni dhahabu ama almasi, je! kila mtu asingekuwa anang\u2019ang\u2019ana sana kuokota kulingana na uwezo wake? Lakini sasa, kwa vile ni mavumbi tu; basi hakuna mwenye haja nayo\u201d. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Je! nayaongelea mavumbi? La, hasha; bali naongea kuhusu sisi wanadamu. Hivyo ndivyo tulivyo katika haya maisha yetu ya kimwili. Hatuna thamani yo yote ile ya kutamanika wala kupiganiwa. Lakini kinyume cha huu ukweli; watu kila mahali ulimwenguni wanapigana kila mmoja akitetea msimamo wake. Kwa nini? Kwa sababu uongo wa Shetani unatuambia kwamba sisi ni kama Mungu, na kwa hivyo mtu asituone wajinga, wala asitufikirie kuwa wanyonge n.k.<br \/>\nNi kwa nini hatuangalii mfano wa wale wapatao ajali za barabarani, au za milipuko ya mabomu, au athari ya kukosa vyakula ama maji? Je! hatuoni jinsi wanavyotawanyika kama mavumbi tu? Ku wapi kule kuwa kama Mungu? Ki wapi kitu cha kupigania katika huu mwili unaotawanyika na kuvunjika kama mayai? Ki wapi kitu cha kutegemea katika utajiri ambao hautupi uhai? Je! utajiri unaweza kutulinda dhidi ya madhara hayo pindi yatupatapo?<br \/>\nHapa ndipo siri ya uongo wa Shetani ilipo. Tumeacha kutafuta ile thamani ambayo Mungu alituahidi <\/span><span class=\"fontstyle3\">(yaani, kutokufa na miili isiyoharibika),<\/span><span class=\"fontstyle2\">na badala yake tukakubaliana na Shetani na tukaanza <\/span><span class=\"fontstyle2\">kujiharibu huku tukidhani kuwa tunajijenga. Tunapaswa tugutuke <\/span><span class=\"fontstyle3\">(tuamke) <\/span><span class=\"fontstyle2\">na tujue kuwa Shetani anataka tujimalize wenyewe; naam, anataka tufe sote kwa kuufuata huo uongo wake. Ili tujitoe hapo, ni lazima tukubali kwamba sisi ni mavumbi, na tumwendee Mungu ili aendelee kutuumba hata tufikie kiwango cha kujivunia na cha kutetea. Lazima pia tukubali kwamba haya maisha ya uongo wa Shetani ndiyo ambayo yanasababisha huu uovu wote uliomo duniani sasa.<br \/>\nKama kila mtu duniani angejikubali kuwa yeye ni mavumbi, na kumwendea Mungu ili aumbwe upya, je! watu wangetofautiana ama kupigania nini? Kama kila mtu angekuwa mwangalifu asidanganywe na Shetani na badala yake amfuate Mungu, je! tofauti kati yake na mwanadamu mwenzake ingetoka wapi? Kwa hali hiyo wapendwa: je! dunia isingekuwa na Amani na furaha isiyo na kifani?<br \/>\nTumshukuru Mungu ambaye kwa upendo wake kwa wanadamu, aliyaona haya mateso yote, na akamtuma mjumbe wake Yesu Kristo ili aje <\/span><span class=\"fontstyle0\">&#8220;atufungue macho ili tutoke katika huo uongo na kuja katika ufahamu wa kweli, tutoke kwenye uharibifu na kuuendea uzima, ili Amani mwishowe iijae dunia yote&#8221;, <\/span><span class=\"fontstyle4\">soma Waefeso2:17-18.<\/span><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle4\"><br \/>\n<\/span><strong><span class=\"fontstyle0\">MGEUKIE MUUMBA WAKO<\/span><\/strong><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle0\"><br \/>\n<\/span><span class=\"fontstyle2\">Tuanzie wapi basi? Tuache kuangaliana na kutafutana sisi kwa sisi; na badala yake tuanze kumwangalia na kumtafuta Muumba wetu ambaye ndiye pekee atakayetuambia ukweli wote kutuhusu. Watu kwa kutokuyafahamu hayo, wameyaacha mafundisho ya Mungu na kujidhania kuwa wenye hekima, ambayo matokeo yake ni kinyume. Mungu anawashangaa akiuliza: <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Mwasemaje, Sisi tuna<br \/>\nakili,&#8230; tazama, wamelikataa neno la Bwana <\/span><span class=\"fontstyle3\">(ambalo ni maisha ya kweli), <\/span><span class=\"fontstyle4\">wana akili gani ndani yao?&#8221; Yeremia 8:8-9. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Na tena: <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;&#8230; ikiwa hawasemi sawasawa na neno hili <\/span><span class=\"fontstyle3\">(sheria za Mungu), <\/span><span class=\"fontstyle4\">bila shaka kwa hao hapana asubuhi <\/span><span class=\"fontstyle3\">(ni giza na ujinga mtupu)&#8221; <\/span><span class=\"fontstyle4\">Isaya 8:20. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Ikiwa basi tunataka kujiepusha na haya maovu na kupata ulinzi kutoka kwa muumba wetu, basi anatuambia; <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Mimi ni Bwana, Mungu wako,<br \/>\nnikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata. Laiti ungalisikiliza amri zangu! Ndipo amani yako ingalikuwa kama mto wa maji, na haki yako kama mawimbi ya bahari&#8221; Isaya 48:17. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Je! tunayaamini haya Mungu ayasemayo hapa? Na kama ndiyo; basi tuanze kwa kujisahau, kuwasahau wanadamu wenzetu, kusahau mila na tamadumi zote ambazo zimejengwa juu ya uongo;<br \/>\nambazo kadiri tunavyong\u2019ang\u2019ana kuzitimiza ili tupate kibali mbele ya wanadamu, tumejiletea shida ambazo sasa zinatishia kutumaliza. Mungu anasema tukubali kwamba, <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Baba zetu hawakurithi kitu ila uongo, naam, ubatili na vitu visivyofaa. Je! Mwanadamu ajifanyie miungu, wasio miungu?&#8221; Yeremia 16:19-20. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Naam; wanadamu walianza kwa kumweka Mungu kando na wakaanza kuangaliana wao kwa<br \/>\nwao na kuabudiana huku wakitegemeana, jambo ambalo Mungu amekataza kabisa akisema; <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha Bwana&#8221; Yeremia 17:5. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Anazidi kuonya akisema, <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Maana BWANA aliniambia hivi, kwa mkono hodari, akanifundisha nisiende katika njia ya watu hawa, akisema, Msiseme, Ni fitina; katika habari za mambo yote ambayo watu hawa watasema, Ni fitina; msihofu kwa hofu yao, wala msiogope. BWANA wa majeshi ndiye mtakayemtakasa; na awe yeye hofu yenu, na awe yeye utisho wenu&#8221; Isaya 8:11-13. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Endapo tutayasikiliza haya maagizo na kuyatii; basi tutaacha kubabaishwa na maneno ya wanadamu na kuacha pia kuyategemea kama hukumu zetu, iwe ni kwa kusifiwa ama kwa kudharauliwa. Maana, ikiwa tunajua vizuri kwamba mtu hana ufahamu wo wote; basi wakati anapokudharau au kukusifu, yote hayo ni udanganyifu tu. Sasa kwa nini utegemee hukumu zake<\/span> <span class=\"fontstyle2\">badala ya kutegemea hukumu za Mungu katika maandiko? Mungu anatuuliza akisema; <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Mimi, naam, mimi, ndimi niwafarijiye; wewe u nani hata ukamwogopa mtu atakayekufa, na mwanadamu atakayefanywa kuwa kama majani? Ukamsahau BWANA, Muumba wako, yeye aliyezitanda mbingu, na kuiweka misingi ya dunia; nawe unaogopa daima mchana kutwa kwa sababu ya ghadhabu yake yeye aoneaye, hapo afanyapo tayari kuharibu; nayo i wapi ghadhabu yake aoneaye?&#8221; Isaya 51:12-13.<\/span><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle4\"><br \/>\n<\/span><span class=\"fontstyle2\">Ikiwa mtu haongei maneno ya Mungu; basi asikubabaishe kwa lo lote, iwe kwamba anakusifu ama kwamba anakudharau, maana anaongea uongo, na tunajua kwamba uongo ni ubatili. Yesu aliyajua hayo na ndiyo sababu alisema kwamba; <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Heri ninyi watu watakapowachukia, na kuwatenga, na kuwashutumu, na kulitupa nje jina lenu kama neno ovu, kwa ajili ya Mwana wa Adamu <\/span><span class=\"fontstyle3\">(kwa ajili ya maisha ya kweli). <\/span><span class=\"fontstyle4\">Furahini siku ile na kuruka-ruka, kwa kuwa, tazama, thawabu yenu ni kubwa mbinguni&#8230;&#8221; Luka 6:22-23. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Tena wakati wanapokusifu <\/span><span class=\"fontstyle3\">(kwa kutokujua kwamba ni Mungu ndiye atendaye wema ndani ya wanadamu: <\/span><span class=\"fontstyle4\">soma Wafilipi 2:13<\/span><span class=\"fontstyle3\">) <\/span><span class=\"fontstyle2\">kwa sababu umetenda yale wayapendayo, je!<br \/>\nufurahie na kukubaliana nao? Na isiwe hivyo. MaanaYesu anatuambia; <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Ole wenu ninyi watu wote watakapowasifu, kwa kuwa baba zao waliwatenda manabii wa uongo mambo kama hayo&#8221; Luka 6:26.<\/span><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle4\"><br \/>\n<\/span><span class=\"fontstyle2\">Kwa nini? Kwani ni vibaya kusifiwa? La, hasha. Lakini uelewe kwamba, mwanadamu wa kimwili husifu tu kile kimpendezacho; na kile kimpendezacho ni ule uongo wa Shetani. Kwa hivyo; mara nyingi, ukiona wanakusifu na kukushangilia, basi ni kwa sababu unafanya mapenzi yao. Kwa maana, ikiwa ni watu wanaomjua Mungu na kusifu kwa haki; basi hawatakusifu wewe bali Mungu. Yesu anayashuhudia hayo akisema; <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Ninyi ndinyi mnaojidai haki mbele ya wanadamu, lakini Mungu awajua mioyo yenu; kwa kuwa lililotukuka kwa wanadamu huwa chukizo mbele za Mungu&#8221; Luka 16:15: soma pia Wakorintho 10:12; Yohana 5:44.<\/span><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle4\"><br \/>\n<\/span><span class=\"fontstyle2\">Kwa hivyo; endapo tutafaulu kujiepusha na huu mpango mbaya wa maisha, tukaanza kwa kujikubali kwamba, sisi ni mavumbi, ni udongo ulio mikononi mwa mfinyanzi <\/span><span class=\"fontstyle3\">(Muumbaji) <\/span><span class=\"fontstyle2\">ambao anaufinyanga ili aweze kumtengeneza mtu aliyetukuka na wa kiroho kama Mungu mwenyewe; tukishajiweka katika hali hiyo, hatutakuwa na cho chote katika huu mwili ambacho tunaweza tukakitetea.<br \/>\nTutavipuuza vyote vya kimwili na kutia jitihada zetu zote katika kuishi kama Mungu na sio kwa kuwaiga wanadamu wenzetu au tamaa za mwili za uharibifu na za kudanganya<\/span><span class=\"fontstyle4\">(soma Waefeso 4:22).<\/span><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle4\"><br \/>\n<\/span><span class=\"fontstyle2\">Ni ndani ya akili za wanadamu ambako vita hupangwa na kuanzia <\/span><span class=\"fontstyle4\">(soma Yakobo 4:1-2). <\/span><span class=\"fontstyle2\">Na kwa hivyo pia, ni hapo ndani ya akili ndipo ambako msingi wa ujenzi wa Amani utakapowekwa. Unahitaji mabadiliko ya nia <\/span><span class=\"fontstyle3\">(akili) <\/span><span class=\"fontstyle2\">na mawazo<\/span><span class=\"fontstyle3\">(mtazamo)<\/span><span class=\"fontstyle2\">ili mabadiliko ya mipango na utendaji pia yafanyike. Huu ndio ujumbe ambao Yesu anawafundisha wote wanaomwamini. Hii ndio habari njema aliyotuletea kutoka<br \/>\nkwa Mungu muumba wetu, na ni kwa ajili ya wanadamu wote. Sasa je! kwa vile tumeyafahamu haya, tuko tayari kubadilika? Je! tuko tayari kuutupilia mbali huu ufahamu wa zamani wote, na kama watoto wadogo, tuanze kujifunza kwa Yesu katika maandiko? Na kama ndiyo; basi hatua ya kwanza ni kutoa mawazo yetu kutoka kwa wanadamu, na kutoka katika mila na tamaduni zao, na tuyaelekeze kwa Mungu<br \/>\naliyetuumba ambaye ndiye peke yake ayafahamuye maisha ya kweli. Tukiishafanya hivyo, hili litabadilisha kila kitu katika maisha yetu. Yale malengo ya kujitahidi kufanya yale ambayo wanadamu wanayataka ili wakupende, ile hali ya kufanya kila kitu kwa kujitazama au kumtazama mwanadamu mwenzako na kuishi kulingana na mila zao, itaondoka. Lengo litakaloanza kutuongoza maishani litakuwa<br \/>\nni lile la kutaka kuufikia uzima wa milele na kufanywa kuwa viumbe wa kiroho kama Mungu.<br \/>\nTukijiweka kwenye hali hiyo, hatutakuwa na kitu cha kung\u2019ang\u2019ania kati yetu. Hatutakuwa na sababu ya kuchukiana au kupigana, maana tutatambua kuwa adui yetu sio mwanadamu mwenzetu, bali ni Shetani aliyemshika mateka kutenda mapenzi yake; na tutaweza kukubaliana na Mungu anavyotuambia kuwa, <\/span><span class=\"fontstyle0\">&#8220;vita vyetu sio dhidi ya damu na nyama <\/span><span class=\"fontstyle3\">(mwanadamu), <\/span><span class=\"fontstyle0\">bali ni dhidi ya pepo wabaya<br \/>\n<\/span><span class=\"fontstyle3\">(mashetani)<\/span><span class=\"fontstyle0\">&#8220;, soma <\/span><span class=\"fontstyle4\">Waefeso 6:12. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Tutafikia katika kiwango cha kutii agizo la Yesu atuambialo kwamba, <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Akuombaye, mpe; naye atakaye kukopa kwako, usimpe kisogo&#8230; Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi&#8221; Mathayo 5:42,44. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Katika hili lengo jipya la maisha, na katika hii akili mpya, utaona kwamba; tabia za wizi, uasherati, unyang\u2019anyi, tamaa mbaya, chuki na mauaji zitaisha.<\/span><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle2\"><br \/>\nNa kufikia hapo rafiki; je! wewe huoni kuwa hii akili mpya ambayo ulimwengu wa leo haunayo ndiyo suluhisho la shida zote zilizoko duniani leo? <\/span><span class=\"fontstyle3\">(kwa maelezo mengine zaidi, agiza ujumbe wetu usemao, <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;MWANADAMU NI NANI?\u201d, <\/span><span class=\"fontstyle3\">ili ujifunze zaidi). <\/span><span class=\"fontstyle2\">Je! huoni kuwa ni kinyume cha ile akili iliyopo hivi sasa? Tukubaliane kwamba, ni Shetani kupitia kwa hii akili ya sasa ya uongo ambaye anawafanya wanadamu kutenda haya maovu yote. Yeye Shetani hatafuti wafuasi, bali anataka kuwadanganya wanadamu, na kwa njia hiyo awafanye kuyakataa maisha ya kweli ili wafe wote. Hii ndiyo sababu unaona wanadamu wanauana kama wanyama; wanatengeneza vitu ambavyo ni hatari sana kwa mazingira. Yote haya ni jitihada za Shetani za kutumaliza kwa kututumikisha kwenye hii akili yake ya udanganyifu. Angalia matokeo yake sasa hivi. Kila taifa duniani leo linakabiliana na upinzani wa aina moja ama nyingine. Vita vinavyosababisha maafa ya maelfu elfu ya watu viko kila mahali. Naam, huyu ni Shetani akitekeleza lengo lake.<\/span><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle2\"><br \/>\nHii ndiyo sababu Mungu kwa huruma zake, ameyaona haya na akaamua kumtuma Yesu, ili atufumbue macho tupate kuiona hii siri ya uongo wa Shetani. Yesu anatukumbusha kwamba, tuko katika huu mwili ili tujifunze kuishi kama Mungu huku tukiyakataa mafundisho ya Shetani, ili kusudi tukishakamilika, tupate kuvikwa miili ya kiroho na kisha tuurithi ufalme wake. Ndiyo sababu alianza kwa kusema, <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Wakati umetimia, na ufalme wa Mungu umekaribia; tubuni, na kuiamini Injili&#8221; Marko 1:15. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Kwa wale watakaousikia wito huu na kuuamini, Mungu anaahidi kuanza kuumba akili yake ndani yao kwa kuziandika amri zake ndani ya mioyo yao ili ziwe ndizo mawazo, fikira na nia za mioyo yao, naam; ziwe ndizo ufahamu wa kutenda cho chote kile mtu atakachotenda katika maisha. Na hili atalifanya<br \/>\nkwa kuwapa roho yake takatifu itakayowawezesha kuyakumbuka haya maagizo yake. Amewaahidi pia ulinzi wake, maana anasema, <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;BWANA atakulinda na mabaya yote, Atakulinda nafsi yako. BWANA atakulinda utokapo na uingiapo, Tangu sasa na hata milele&#8221; Zaburi 121:7-8. <\/span><span class=\"fontstyle2\">Ni kwa kuishi kulingana na hii akili ya Mungu ndiko ambako kutaleta Amani, na ni baada ya kuwa akili zote za wanadamu<br \/>\nzimeigeukia katika wakati ule ambao ufalme wa Mungu utaanza kuitawala dunia hii, na huku pia Shetani akiwa ameondolewa. Kuhusu wakati huo ujao, Mungu anasema, <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Miisho yote ya dunia itakumbuka, Na watu watamrejea BWANA; Jamaa zote za mataifa watamsujudia. Maana ufalme una BWANA; Naye ndiye awatawalaye mataifa&#8221;, soma Zaburi 22:27-31.<\/span><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle4\"><br \/>\n<\/span><span class=\"fontstyle2\">Wapendwa wetu; hili ndilo tumaini la wanadamu. Na hii ndio njia pekee ya kuleta Amani duniani; ni kwa kuimarishwa kwa ufalme wa Mungu, na kuondolewa kwa Shetani ambaye kwa sasa hivi ameushika ulimwengu mateka akijaribu kutekeleza ndoto yake ya kuwaua wanadamu wote. Kuhusiana na wakati huo ujao, Mungu anasema: <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;Na mataifa mengi watakwenda na kusema, Njoni, twende juu<br \/>\nmlimani kwa BWANA, nyumbani kwa Mungu wa Yakobo, naye atatufundisha njia zake, nasi tutakwenda katika mapito yake&#8230;&#8221; <\/span><span class=\"fontstyle2\">Hebu na tulifahamu jambo hili hapa kwamba; baada ya kila mmoja kuanza kujifunza kuishi kama asemavyo Mungu; wakati ambapo serikali ya Mungu itakuwa imeimarishwa, na mji wake mkuu ukiwa Yerusalemu; naam, wakati ambapo <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;sheria itatoka Sayuni, na neno la BWANA kutoka Yerusalemu&#8221; <\/span><span class=\"fontstyle2\">huku BWANA mwenyewe <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;akiwahukumu mataifa\u201d, <\/span><span class=\"fontstyle2\">je! kutatokea nini? Nia na mawazo ya watu yatabadilika, <\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;.\u2026nao watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao iwe miundu; taifa halitainua upanga juu ya taifa lingine, wala hawatajifunza vita tena<br \/>\nkamwe&#8221; Isaya 2:3-4. <\/span><span class=\"fontstyle3\">(kwa maelezo ya kina zaidi, basi agiza kitabu chetu kisemacho,<\/span><span class=\"fontstyle4\">&#8220;UFALME WA MBINGUNI&#8221;,<\/span><span class=\"fontstyle3\">ili ujifunze zaidi).<\/span><br \/>\n<span class=\"fontstyle2\">Sasa je! mpendwa; Wewe ni miongoni mwa wale wanaoitafuta hii Amani ya kweli, na ungependa kuwa miongoni mwa wale wanaojitayarisha kwa ajili yake? Wajumbe wa Mungu wako hapa tayari kukujulisha mengi. Na huduma hii inatolewa kwako bure kabisa pasipo malipo yo yote yale utakayotozwa. Ni kazi ya Mungu na wala si ya mwanadamu. Unachohitaji kufanya ni kuwasilina nasi<br \/>\nkwa anuani zetu zilizopo hapa chini, nasi tutakuhudumia bure.<\/span><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle2\"><br \/>\nTunavyo vijarida na vitabu vingi na vyenye mada mbali mbali vitolewavyo bure kwa ajili yako. Baadhi ya vijarida vyetu ni kama vile; <\/span><\/p>\n<ul>\n<li><span class=\"fontstyle2\">JE, WEWE NI MKRISTO?, <\/span><\/li>\n<li><span class=\"fontstyle2\">KUOKOLEWA KWA NEEMA,<\/span><\/li>\n<li><span class=\"fontstyle2\">KWANINI SHERIA?, <\/span><\/li>\n<li><span class=\"fontstyle2\">THAMANI YA UKRISTO, <\/span><\/li>\n<li><span class=\"fontstyle2\">KANISA LA SIKU ZA MWISHO, <\/span><\/li>\n<li><span class=\"fontstyle2\">JE! KRISTO<\/span><\/li>\n<li><span class=\"fontstyle2\">AMEGAWANYIKA?, <\/span><\/li>\n<li><span class=\"fontstyle2\">SHERIA ZA KIAFYA, <\/span><\/li>\n<li><span class=\"fontstyle2\">ROHO YA SABATO ZA MUNGU,<\/span><\/li>\n<li><span class=\"fontstyle2\">MWANADAMU NI NANI n.k.<\/span><\/li>\n<\/ul>\n<p><span class=\"fontstyle2\"><br \/>\nBaadhi ya vitabu vyetu pia ni kama vile; <\/span><\/p>\n<ul>\n<li><span class=\"fontstyle2\">UFALME WA MBINGUNI, <\/span><\/li>\n<li><span class=\"fontstyle2\">KIFO NA KIYAMA, <\/span><\/li>\n<li><span class=\"fontstyle2\">SIKUKUU ZA MUNGU, <\/span><\/li>\n<li><span class=\"fontstyle2\">AMRI KUMI, <\/span><\/li>\n<li><span class=\"fontstyle2\">DINI ZA MITINDO, <\/span><\/li>\n<li><span class=\"fontstyle2\">BIBLIA NA AFYA ZETU, <\/span><\/li>\n<li><span class=\"fontstyle2\">KUFA NA KUFUFUKA KWA YESU, <\/span><\/li>\n<li><span class=\"fontstyle2\">MISINGI YA IMANI YA KANISA LA MUNGU n.k.<br \/>\n<\/span><\/li>\n<\/ul>\n<p><span class=\"fontstyle2\">Agiza sasa kile\/vile utakavyopenda kujifunza, nasi tutakutumia huko ulipo bure kabisa. Wasiliana<br \/>\nnasi kwa anuani zifuatazo:-<br \/>\n<\/span><span class=\"fontstyle0\">KANISA LA MUNGU \u2013 TANZANIA<br \/>\nNambari za simu; +255 753 359 179, +255 688 359 179 na +255 655 659 179<br \/>\nBarua pepe; <\/span><span class=\"fontstyle4\">Ukweliwabiblia@yahoo.com.sg<br \/>\n<\/span><\/p>\n<p><span class=\"fontstyle0\">KANISA LA MUNGU &#8211; KENYA<br \/>\nBarua pepe; <\/span><span class=\"fontstyle4\">endcog@gmail.com<br \/>\n<\/span><span class=\"fontstyle4\">Neema na iwe kwenu na amani zitokazo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo.<br \/>\nUtukufu una yeye tangu milele, sasa na hata milele; Amina.<\/span><\/p>\n","protected":false},"excerpt":{"rendered":"<p>Tunaishi katika ulimwengu ambao ni wachache sana wanaoufahamu. Muulize mtu ye yote yule kuhusu cho chote kile kihusucho maisha, majibu utakayopata yatakuwa ni ya kubahatisha tu; hayana uthabiti wo wote. Mashirika yetu ya uma yana tamaduni na mila zinazotumika kuongoza watu katika namna ya kuishi na kuhusiana wao kwa wao. Ukiziangalia hizi tamaduni na mila,&#8230;<\/p>\n","protected":false},"author":1,"featured_media":0,"comment_status":"open","ping_status":"open","sticky":false,"template":"","format":"standard","meta":{"footnotes":""},"categories":[4],"tags":[],"class_list":["post-159","post","type-post","status-publish","format-standard","hentry","category-swahili-messages"],"yoast_head":"<!-- This site is optimized with the Yoast SEO plugin v22.0 - https:\/\/yoast.com\/wordpress\/plugins\/seo\/ -->\n<title>HUYU NI SHETANI! - End-time Church of God<\/title>\n<meta name=\"robots\" content=\"index, follow, max-snippet:-1, max-image-preview:large, max-video-preview:-1\" \/>\n<link rel=\"canonical\" href=\"https:\/\/endtimecog.org\/html\/huyu-ni-shetani\/\" \/>\n<meta property=\"og:locale\" content=\"en_US\" \/>\n<meta property=\"og:type\" content=\"article\" \/>\n<meta property=\"og:title\" content=\"HUYU NI SHETANI! - End-time Church of God\" \/>\n<meta property=\"og:description\" content=\"Tunaishi katika ulimwengu ambao ni wachache sana wanaoufahamu. Muulize mtu ye yote yule kuhusu cho chote kile kihusucho maisha, majibu utakayopata yatakuwa ni ya kubahatisha tu; hayana uthabiti wo wote. Mashirika yetu ya uma yana tamaduni na mila zinazotumika kuongoza watu katika namna ya kuishi na kuhusiana wao kwa wao. Ukiziangalia hizi tamaduni na mila,...\" \/>\n<meta property=\"og:url\" content=\"https:\/\/endtimecog.org\/html\/huyu-ni-shetani\/\" \/>\n<meta property=\"og:site_name\" content=\"End-time Church of God\" \/>\n<meta property=\"article:publisher\" content=\"https:\/\/www.facebook.com\/endtimecog\" \/>\n<meta property=\"article:published_time\" content=\"2017-02-17T09:54:26+00:00\" \/>\n<meta name=\"author\" content=\"james\" \/>\n<meta name=\"twitter:card\" content=\"summary_large_image\" \/>\n<meta name=\"twitter:label1\" content=\"Written by\" \/>\n\t<meta name=\"twitter:data1\" content=\"james\" \/>\n\t<meta name=\"twitter:label2\" content=\"Est. reading time\" \/>\n\t<meta name=\"twitter:data2\" content=\"24 minutes\" \/>\n<script type=\"application\/ld+json\" class=\"yoast-schema-graph\">{\"@context\":\"https:\/\/schema.org\",\"@graph\":[{\"@type\":\"WebPage\",\"@id\":\"https:\/\/endtimecog.org\/html\/huyu-ni-shetani\/\",\"url\":\"https:\/\/endtimecog.org\/html\/huyu-ni-shetani\/\",\"name\":\"HUYU NI SHETANI! - End-time Church of God\",\"isPartOf\":{\"@id\":\"https:\/\/endtimecog.org\/html\/#website\"},\"datePublished\":\"2017-02-17T09:54:26+00:00\",\"dateModified\":\"2017-02-17T09:54:26+00:00\",\"author\":{\"@id\":\"https:\/\/endtimecog.org\/html\/#\/schema\/person\/712ee17a931abb36c2b2fcf1530cccfc\"},\"inLanguage\":\"en-US\",\"potentialAction\":[{\"@type\":\"ReadAction\",\"target\":[\"https:\/\/endtimecog.org\/html\/huyu-ni-shetani\/\"]}]},{\"@type\":\"WebSite\",\"@id\":\"https:\/\/endtimecog.org\/html\/#website\",\"url\":\"https:\/\/endtimecog.org\/html\/\",\"name\":\"End-time Church of God\",\"description\":\"\",\"potentialAction\":[{\"@type\":\"SearchAction\",\"target\":{\"@type\":\"EntryPoint\",\"urlTemplate\":\"https:\/\/endtimecog.org\/html\/?s={search_term_string}\"},\"query-input\":\"required name=search_term_string\"}],\"inLanguage\":\"en-US\"},{\"@type\":\"Person\",\"@id\":\"https:\/\/endtimecog.org\/html\/#\/schema\/person\/712ee17a931abb36c2b2fcf1530cccfc\",\"name\":\"james\",\"image\":{\"@type\":\"ImageObject\",\"inLanguage\":\"en-US\",\"@id\":\"https:\/\/endtimecog.org\/html\/#\/schema\/person\/image\/\",\"url\":\"https:\/\/secure.gravatar.com\/avatar\/904dfea7a9a2673e22a19f8c34f45d6c9a987b99451567ea0c2e728ed363cded?s=96&d=mm&r=g\",\"contentUrl\":\"https:\/\/secure.gravatar.com\/avatar\/904dfea7a9a2673e22a19f8c34f45d6c9a987b99451567ea0c2e728ed363cded?s=96&d=mm&r=g\",\"caption\":\"james\"},\"sameAs\":[\"http:\/\/endtimecog.org\/html\"],\"url\":\"https:\/\/endtimecog.org\/html\/author\/james\/\"}]}<\/script>\n<!-- \/ Yoast SEO plugin. -->","yoast_head_json":{"title":"HUYU NI SHETANI! - End-time Church of God","robots":{"index":"index","follow":"follow","max-snippet":"max-snippet:-1","max-image-preview":"max-image-preview:large","max-video-preview":"max-video-preview:-1"},"canonical":"https:\/\/endtimecog.org\/html\/huyu-ni-shetani\/","og_locale":"en_US","og_type":"article","og_title":"HUYU NI SHETANI! - End-time Church of God","og_description":"Tunaishi katika ulimwengu ambao ni wachache sana wanaoufahamu. Muulize mtu ye yote yule kuhusu cho chote kile kihusucho maisha, majibu utakayopata yatakuwa ni ya kubahatisha tu; hayana uthabiti wo wote. Mashirika yetu ya uma yana tamaduni na mila zinazotumika kuongoza watu katika namna ya kuishi na kuhusiana wao kwa wao. Ukiziangalia hizi tamaduni na mila,...","og_url":"https:\/\/endtimecog.org\/html\/huyu-ni-shetani\/","og_site_name":"End-time Church of God","article_publisher":"https:\/\/www.facebook.com\/endtimecog","article_published_time":"2017-02-17T09:54:26+00:00","author":"james","twitter_card":"summary_large_image","twitter_misc":{"Written by":"james","Est. reading time":"24 minutes"},"schema":{"@context":"https:\/\/schema.org","@graph":[{"@type":"WebPage","@id":"https:\/\/endtimecog.org\/html\/huyu-ni-shetani\/","url":"https:\/\/endtimecog.org\/html\/huyu-ni-shetani\/","name":"HUYU NI SHETANI! - End-time Church of God","isPartOf":{"@id":"https:\/\/endtimecog.org\/html\/#website"},"datePublished":"2017-02-17T09:54:26+00:00","dateModified":"2017-02-17T09:54:26+00:00","author":{"@id":"https:\/\/endtimecog.org\/html\/#\/schema\/person\/712ee17a931abb36c2b2fcf1530cccfc"},"inLanguage":"en-US","potentialAction":[{"@type":"ReadAction","target":["https:\/\/endtimecog.org\/html\/huyu-ni-shetani\/"]}]},{"@type":"WebSite","@id":"https:\/\/endtimecog.org\/html\/#website","url":"https:\/\/endtimecog.org\/html\/","name":"End-time Church of God","description":"","potentialAction":[{"@type":"SearchAction","target":{"@type":"EntryPoint","urlTemplate":"https:\/\/endtimecog.org\/html\/?s={search_term_string}"},"query-input":"required name=search_term_string"}],"inLanguage":"en-US"},{"@type":"Person","@id":"https:\/\/endtimecog.org\/html\/#\/schema\/person\/712ee17a931abb36c2b2fcf1530cccfc","name":"james","image":{"@type":"ImageObject","inLanguage":"en-US","@id":"https:\/\/endtimecog.org\/html\/#\/schema\/person\/image\/","url":"https:\/\/secure.gravatar.com\/avatar\/904dfea7a9a2673e22a19f8c34f45d6c9a987b99451567ea0c2e728ed363cded?s=96&d=mm&r=g","contentUrl":"https:\/\/secure.gravatar.com\/avatar\/904dfea7a9a2673e22a19f8c34f45d6c9a987b99451567ea0c2e728ed363cded?s=96&d=mm&r=g","caption":"james"},"sameAs":["http:\/\/endtimecog.org\/html"],"url":"https:\/\/endtimecog.org\/html\/author\/james\/"}]}},"_links":{"self":[{"href":"https:\/\/endtimecog.org\/html\/wp-json\/wp\/v2\/posts\/159","targetHints":{"allow":["GET"]}}],"collection":[{"href":"https:\/\/endtimecog.org\/html\/wp-json\/wp\/v2\/posts"}],"about":[{"href":"https:\/\/endtimecog.org\/html\/wp-json\/wp\/v2\/types\/post"}],"author":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/endtimecog.org\/html\/wp-json\/wp\/v2\/users\/1"}],"replies":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/endtimecog.org\/html\/wp-json\/wp\/v2\/comments?post=159"}],"version-history":[{"count":0,"href":"https:\/\/endtimecog.org\/html\/wp-json\/wp\/v2\/posts\/159\/revisions"}],"wp:attachment":[{"href":"https:\/\/endtimecog.org\/html\/wp-json\/wp\/v2\/media?parent=159"}],"wp:term":[{"taxonomy":"category","embeddable":true,"href":"https:\/\/endtimecog.org\/html\/wp-json\/wp\/v2\/categories?post=159"},{"taxonomy":"post_tag","embeddable":true,"href":"https:\/\/endtimecog.org\/html\/wp-json\/wp\/v2\/tags?post=159"}],"curies":[{"name":"wp","href":"https:\/\/api.w.org\/{rel}","templated":true}]}}